Total Pageviews

Tuesday, 22 December 2015

PROGRAMU MPYA YA ‘PANDA MITI KIBIASHARA’ YAANZISHWA NCHINI

Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi ya Finland imeanzisha Programu ya ’Panda Miti Kibiashara’ (Private Forestry Programme).

Programu hiyo yenye makao makuu Njombe inayo madhumuni ya kuwahamasisha wananchi kupanda miti kwa kuzingatia kuwa miti ni zao la biashara.

Ingawaje Programu hiyo imeshiriki kwa mara ya kwanza katika maonyesho ya Sabasaba ilikuwa kati ya sehemu zilizowavutia watu wengi ndani banda la Maliasili na Utalii. Wananchi waliotembelea waliuliza maswali kuhususiana na aina za miti ya mbao inayofaa kupandwa katika sehemu zao na upatikanaji wake.

Programu ya Panda Miti Kibiashara inatekelezwa katika wilaya sita za Ludewa, Makete, Njombe, Kilolo, Mufindi na Kilombero. Programu hii ni ya miaka 16 lakini itatekelezwa kwa awamu za miaka minne kila moja.


Lengo la Programu hiyo  ni  kuongeza kipato cha wananchi  waishio  vijijini kwa kupanda miti. Lengo hilo litafanikiwa kama wananchi watalima mashamba ya miti kitaalamu kwa kuzingatia matumizi  ya  mbegu bora na kulihudumia shamba kitaalamu ili mazao yatakayopatikana  yaweze kuvutia soko la ndani na nje.



Lengo lingine ni kuanzisha shughuli  ya kujiongezea kipato nje ya shamba la miti wakati wahusika wakisubiri miti ifikie umri wa kuvunwa. Shughuli hizo ni kama vile kilimo cha matunda na ufugaji nyuki. Aidha wananchi  wamehimizwa kuunda vikundi vya Wakulima wa Miti ili iwe rahisi kwa Programu kutoa msaada kwao.
Kwa sasa miche ambayo itapandwa na wananchi walioko katika wilaya zinazohudumiwa na Programu inakuzwa kwenye vitalu ili iwe tayari kupandwa mwezi Desemba mwaka huu na Januari mwakani.
Programu imeazimia kuwa katika kipindi cha awamu ya kwanza ya Programu (mwaka 2014 hadi 2017) jumla ya hekta 15,000 zitapandwa na wananchi waliojiunga na Vikundi vya Wakulima wa Miti.






UFUGAJI BORA WA SUNGURA









UTANGULIZI
Kabla hujaamua kufuga sungura hakikisha ya kwamba umejitoa na una muda wa kuwahudumia wanyama hawa, ufugaji wao si rahisi kama vile ukifuga paka au mbwa, sungura wanahitaji uangalizi na hasa kwenye usafi kwa sababu ni rahisi kwao kupata maradhi yatokanayo na mazingira mabaya na machafu


MABANDA
Kuna aina mbili za mabanda ya kufugia kwanza ni yale ya kuwafungia ndani muda wote bila kutoka nje na ya pili ni ile ya pili ni nusu nusu yaani wanakuwa na mabanda na wanaweza kutoka nje kwenye ua maalumu, katika aina zote mbili ni muhimu kuhakikisha hakuna upenyo wa kuruhusu panya kupita kwa sababu huwa wanakula watoto wa sungura


UFUGAJI WA NDANI
1 - Usitumie banda la kioo (aquarium) kwa sababu halina hewa ya kutosha na ni vigumu kusafisha

2 - Sakafu ya nyavu za waya ni nzuri zaidi ila hakikisha hakuna sehemu zenye ncha kali inayoweza kuwaumiza sungura, kwani wakiumia ni mpaka wapone wenyewe au umchinje kwa sababu ukitumia dawa za antibiotic sungura mwili wake hauna uwezo wa kuzimeng'enya na kuisha mwilini mwake, siku ukimchinja atabakia na dawa na hata ukinusa nyama yake utahisi harufu ya dawa

3 - Ukubwa wa banda usipungue mita 4 kwa 2 kwa kila sungura mmoja, likiwa kubwa zaidi ni vizuri

4 - Weka  matandazio kama nyasi kavu au maranda ya mbao, lakini maranda yatokanayo na miti yenye mafuta kama mi-pine na mikaratusi hayafai, wawekee kipande cha blanket au taulo  kwa ajili ya kulalia na kuzalia hasa kwa wazazi

5 - Ni muhimu kuwawekea sehemu ya kujificha mara wanapohisi hatari, unaweza kutumia mbao, box gumu au plastiki


UFUGAJI WA NJE
1 - Sehemu yote izungushiwe wavu wa kuku kuzuia panya kuingia na wanyama wengine kama paka, mbwa, mwewe nk

2 - Upande mmoja uwe na mabanda, sehemu ya chakula na maji pamoja na kivuli kwa ajili ya sungura kupumzika

3 - Futi moja chini ya udongo kuwe na zege kuzuia sungura kuchimba na kwenda mbali

4 - Eneo la wazi liwe huru na hatari zote za sumu kama dawa za kuulia wadudu au mbolea, pia majani yaliyoota yasiwe ni yale yenye sumu (waone wataalamu wakushauri au ng'oa yote)

MAJI
Tumia mabakuli ya kigae, plastiki au jengea kwa saruji, maji yabadilishwe kila siku na vyombo visafishwe kila siku

CHAKULA
Wapewe majani, mabaki ya mboga za jikoni baada ya kuchambuliwa, pia unaweza kuwawekea pumba au chakula cha kuku (growers mash) kwenye vyombo maalumu kama chakula chenye virutubisho (concentrates)

USAFI
Kila siku ondoa uchafu kama vyakula vilivyo mwagika, na kinyesi kilichoganda kwenye matandazio, fagia na kubadili matandazio angalau mara moja kwa wiki, manyoya ya sungura mzazi yasiondolewe hii huonyesha kwamba anakaribia kuzaa watoto


MENO
Wakati mwingine meno ya mbele hukua sana na kumsababishia usumbufu wakati wa kula, waone wataalamu ukiona ni marefu zaidi na yanahitaji kupunguzwa, dalili kuu ni sungura kushindwa kula kwa zaidi ya saa 12

MIGUU
Miguu ya sungura si kama ya wanyama wengine, nyayo zake zimefunikwa kwa manyoya, angalia ukiona yananyonyoka kuna tatizo chunguza, kucha zake nazo huhitaji kupunguzwa zikikua sana

UBEBAJI
Usimbebe kwa kutumia masikio yake huwa wanaumia sana, shika ngozi nyuma ya shingo kama paka ukitaka kumbeba


Usimbebe Hivi Sungura wako







Sungura anatakiwa kubebwa hivi







DAWA
Wapewe dawa ya minyoo kama Piperazine kila baada ya miezi mitatu, dawa za wadudu kama Akheri Powder zinyunyuziwe kwenye mabanda yao kuzuia viroboto, usiwape dawa nyingine bila ushauri wa kitaalamu, antibiotics ndio usijaribu kabisa.



KUROILER

Kuroiler ni kuku wenye asili ya india na zifuatazo ni sifa zao.


1. Wanafugwa kienyeji (ni kuku wa kienyeji au una weza kuwafuga kisasa kwa kuwaweka ndani ya banda ila wawe free)




2. Hawapati magonjwa kirahisi



3. Wanaanza kutaga wakiwa na miezi 5 



4. Wanataga miaka miwili.



5. Majogoo yanafika hadi kilo 5 na mitetea 3.5kg hadi 4kg



6. Wanataga mayai 250 na zaidi kwa mwaka. 



7. Mayai yake ni fertile ila hawalalii.  Mayai hutotoleshwa kwa incubators. 


8.  Wana nyama nyingi.

  


Wasiliana nasi 0765903379, upate kuunganishwa na wauzaji;

wanauzwa kwa order Kifaranga kimoja ni shilingi 2,500/=, kuanzia vifaranga  100 na kuendelea.


Mayai ya Kuroiler


Kuroiler




Mfugaji Witness


Mfugaji Witness Rweyemamu akiwa bandani, anafuga kuku wa nyama (broiler) huko Vikawe.  Ana kuku zaidi ya 1,000.
Kwa Mawasiliano ya Manunuzi wasiliana naye kwa simu namba 0712466711

Friday, 18 December 2015

MAWAZO YANAPOFANYIWA KAZI - USHUHUDA WA MAWAZO KWENDA VITENDO


Sophie Kessy - Mkulima wa Vitunguu
Ni Mwanachama na Mkulima  pia Mtangazaji wa Clouds

Asante Mungu nauona utukufu wako ...asante mwanangu kwa moyo wa kusimamia shuhuli hii sio ndogo baba am so happy and proud of you Tariq Ferreje inshalah Mungu ni mwema...we are almost there Buberwa Robert




Napenda kuchukua nafasi hii kukupongeza wewe dada Sophie Kessy kwa usikivu wako, nakumbuka siku ya kwanza ulipoomba ushauri, hadi ukakumbwa na mafuriko ambapo eneo kubwa lilisombwa na maji na kiasi kikubwa cha mazao kuchukuliwa na maji, ulinipigia na kuniomba ushauri na nilikushauri bila ya hiyana ulifanya kwa kupitia ushauri wangu na wa wadau wengine.

Wewe ni mfano wa kuigwa kwa kuwa uliamua kufuata maelekezo na sasa unaonekana shujaa.  Nafurahi sana wewe ni moja ya wapiganaji wangu.  Naomba wamama na wadada wengine mufuate  ujasiri huu naamini mtafanikiwa.

Hongera sana Sophie Kessy.




NEEMA DANDA - 0652003630









NEEMA DANDA Mwanachama na Mfugaji wa;
Kuku wa Kienyeji
Kuku wa Nyama
Kuku wa Mayai

Anapatikana Kimara - Suka


Thursday, 17 December 2015

HYDROPONIC FODDER














Ni teknolojia ya kuotesha mazao kwa maji na virutubisho bila kutegemea udongo.

Ni kimea kinachooteshwa kwa kutumia mbegu za shayiri, ili kupata chakula cha mifugo, Ng'ombe, kuku, mbuzi,kondoo, nguruwe.

Ni kilimo kinachohitaji eneo dogo, maji kidogo, hakuna haja ya udongo.

FAIDA

Ni rahisi kufanya kilimo hiki mahali popote.  Husaidia kuvuna na kupata mazao mengi kwa muda wa siku 7 pia inapunguza matumizi ya fedha kwa kununua majani, pumba kwa ndege na wanyama.

Haona madhara kwa afya za wanyama na ndege.

ULIMAJI

Kilimo hiki kinahitaji;
1. Banda maalumu la ukubwa wowote.
2. Trei za plastiki au aluminiam zenye matundu (hakikisha zisiwe na material inayozalisha kutu)
3. Virutubisho kama vile Di.Grow (green)
4. Chupa za kunyunyizia maji (sprayer)
5. Mbegu za shayiri au ngano (zisiwe zimeshambuliwa na wadudu)
6. Chombo la kulowka mbegu
7. Kitambaa cheupe




Jaribio nililofanya mwenyewe 





mbuzi akila 


ng'ombe akila


kondoo akila

 Trei 



eneo dogo mavuno mengi












CHANGAMKA MKULIMA 

Kwa mawasiliano 
+255765903379
buberwamujuni@gmail.com

Facebook: FREBU Poultry Farm Page