Total Pageviews

Wednesday 3 February 2016

Kilimo cha Maua



Ndugu Wapetani, kuna haja kubwa sana kwetu kuwa wabunifu na kuweza kuifanya biashara yetu hii kuwa yenye mvuto na tija kwetu.  Nasema haya kwa kuwa tumekuwa kama tumejisahau kidogo kwa kukaa na kusubiri wateja waje katika maeneo ya biashara zetu ili kutupa mia mbili mia tatu, tuna ishusha thamani biashara hii.  Hebu tutafute njia ya kulipendezesha jiji kwa kuingia mikataba maeneo mengi kwa ku design maeneo mengi na kuweka maua pamoja na miti,  tuandike miradi yetu na kuweka faida za kuwa na bidhaa zetu katika jiji hili la Dar es Salaam na Wilaya zake, tuwabadili fikra wakazi wa Dar kwa kuwa wekea mazingira mazur na si mabiwi ya takataka tunazoona na harufu mbaya tunayoinusa kila kukicha.  Ni wakati sasa wa kubadilika na kulitengeneza jiji.

Hivi ni lini mara ya mwisho umewaona vipepeo wazuri katika macho yako wakikatisha mbele ya macho yako zaidi ya inzi wa aina mbili, kama sio yule wa chooni , basi yule wa majalalani na katika vidonda na vinyesi anayetuletea magonjwa kama kipindupindu na maradhi mengine ya kijingajinga.

Tutumie fursa hii sasa ili kujiingizia kipato lakini pia kulipendezesha jiji.

Jiji la Dar tunaambiwa hakuna mashamba lakini tunaweza kuwa na mashamba ya maua na kuzalisha ajira kwa kulima, kuhifadhi na kuuza maua bila ya kuharibu taratibu za jiji.

Hii ni njia nzuri ya kuwavutia hata wadau na kuanza kuifanya hii biashara kuwa ajira, tena ajira yenye tija kwa wakulima kufanya biashara ndani na nje ya nchi.




Tuchukue mfano wa majirani zetu Kenya wao inakadiriwa zaidi ya Wakenya 500,000 wamejiajiri katika biashara hii, na wameajiri zaidi ya wafanyakazi 90,000 katika mashamba yao.

Mwaka 2013 tani zipatazo 125,000 za maua zilisafirishwa nje ya nchi na kuwaingizia kiasi cha dola za kimarekani 507 milioni ( kiasi cha shilingi za kitanzania 1,110,330,000,000/=) (Trilioni 1.1).

Kiasi cha 25.3% ya pato la Kenya hutokana na kilimo kwa ujumla, na kilimo cha maua kinachangia 1.3%

Wenzetu wakenya 35% ya maua, wanauza ulaya hasa nchi za Holland, Germany, UK, na nyinginezo.  Pia Kenya wana mashamba 127 yanayotambulika na kufanya biashara kimataifa.

Ni wajibu wetu wafanyabiashara wa kilimo hiki tuwe wbunifu na tushirikiane katika kuleta maendeleo yetu binafsi na ya taifa kwa ujumla.  Ukilitenga taifa kwa kutaka biashara iwe yako kama kisiwa hutapiga hatua zaidi ya kuishia kulaumu na kuona kama vile hii sio ajira yenye kuhitaji kulipwa mshahara mnono.

Twaweza jadiliana kwa wale wanaotaka tujiunge kwa pamoja na kuifanya biashara hii kuwa ajira rasmi itakayotuingizia kipato kikubwa kwetu na kwa taifa.  Jiunge nami kwa  WhatsApp namba +255765903379 FREBU Farm Group

2 comments:

  1. Nipeipenda hi blog. binafsi napenda kilimo cha maua (real estate ) for passive income. kilimo hichi kinalipa sana.

    ReplyDelete
  2. Safi,natamani sana kilimo cha maua hasa upatikanaji wa mbegu

    ReplyDelete